
Urusi, ambayo imekuwa ikiisaidia serikali ya Rais Assad kwa hali na mali, imepinga madai kwamba Rais Assad anafaa kuondolewa madarakani.
Lakini baada ya kuzungumza na Waziri wa Mashauri ya Nchi za Nje wa Marekani, Hillary Clinton, Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Urusi, Sergei Lavrov, alishikilia kwamba kuna matumaini makubwa ya kupata makubaliano.
Bi Clinton kwa uapnde wake alisema bado kuna tofauti na matatizo baina yao.
Habari kwa hisani ya BBC Swahili
No comments:
Post a Comment