Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngasa, akiruka kupiga mpira wa kichwa na kufunga bao la pili katika dakika ya 13, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania bara unaoendelea hivi sasa kwenye Uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam. Mabao mawili yamefungwa na Ngasa ambapo goli la kwanza akifunga katika dakika ya 4 kwa suti kali alilopiga akiwa nje ya 18 baada ya pasi nzuri ya Didier Kavumbagu. Bao la tatu limefungwa na beki wa kushoto wa yanga, Oscar Joshua, katika dakika ya 50.
Kipa wa JKT Ruvu, akishangaa na kulalamika na mabeki wake baada ya kufungwa bao la pili.
Mrisho Ngasa, akishangilia bao lake la pili, akipewa kampani na beki wake Canavaro.



No comments:
Post a Comment