Habari za Punde

*RAIS WA ZANZIBAR AWASILI DODOMA LEO KUHUDHURIA KIKAO CHA KAMATI KUU

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk.Rehema Nchimbi mara alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Dodoma leo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na viongozi mbali mbali wa Chama cha Mapinduzi alipowasili katika uwanja wa   Ndege wa Dodoma leo akihudhuria katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kinachoanza jioni hii,(kulia) Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk.Rehema Nchimbi.
 Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM Makao  Makuu Dodoma wakimkaribisha  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein   alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Dodoma leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) akiimba wimbo wa Chama alipokaribishwa na Vijana wa kwaya wa Wilaya ya Dodoma alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma Mjini leo akishiriki katika kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC). Picha na Ramadhan Othman,Dodoma

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.