Habari za Punde

*DAKIKA 90 ZIMEMALIZIKA UWANJA WA TAIFA YANGA YALAZIMISHWA SARE NA ETOILE DU SAHEL 1-1

 Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa, akimtoka beki wa Etoile Du Sahel, wakati wa mchezo wa Kombe la Shirikisho, uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Yanga imelazimishwa sare na waarabu hao wa Tunisia, ambapo Yanga walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 1, lililofungwa na Naidir Haroub 'Canavaro' kwa mkwaju wa penati baada ya Simon Msuva kuchezewa rafu katika eneo la hatari. Bao la Etoile Du Sahel, lilifungwa na ....katika dakika ya 
****************************************
Na Ripota wa Sufianimafoto, Dar es Salaam
 Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kombe la Shirikisho, Yanga  wanakabiliwa na kibarua kigumu kusonga mbele hatua ya mwisho ya mtoano baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya Etoile Du Sahel ya Tunisia.

anga ya Jijini Dar es Salaam, itakuwa na kibarua kigumu katika mchezo wake wa marudiano na timu ya Etoile Du Sahel unaotarajiwa kuchezwa baada ya wiki mbili huko Tunisi, baada ya leo kulazimishwa sare na waarabu hao ya bao 1-1 katika mchezo uliokuwa mgumu kwa timu zote huku waarabu wakionekana kushambulia kwa kijihami zaidi dakika zote.

Yanga inatakiwa kushinda au kutoka sare ya mabao kuanzia mawili katika mchezo wa marudiano uliopangwa kufanyika mjini Tunis wiki mbili zijazo. Endapo timu hiyo itatoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu hiyo, italazimika kupigiana penati ili kumtafuta mshindi.

Tofauti na michezo mengine iliyopita dhidi ya BDF XI ya Botswana na FC Platinum ya Zimbabwe, Yanga ilicheza vizuri katika mechi zote mbili, lakini  katika mchezo dhid ya Etoile, vijana hao wa Jangwani walishindwa kufurukuta richa ya kuongoza kwa bao 1-0 hadi mapumziko.

Yanga ilianza mchezo kwa kasi na kupata bao kwa njia ya penati katika dakika ya pili baada ya kipa wa Etoile, Mathlouthi Aymen kumwangusha Simon Msuva ambaye tayari alikuwa amempiga chenga na kujianda kufunga.

Nahodha wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na ile ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) alifunga penati hiyo. Etoile ilisawazisha katika dakika ya 47 kupitia kwa Ben  Amor Med Amine ambaye alipiga shuti nje ya eneo la hatari na kumpita kipa wa Yanga Ali Mustafa.
 Beki wa Etoile, akimdhibiti mshambuliaji wa Yanga, Amis Tambwe.
 Amis Tambwe, akijilaumu baada ya kukosa bao.....
 Mashabiki wa Etoile, wakishangilia bao la timu yao.....
Amis Tambwe, akiwania mpira na beki wa Etoile. KATIKA MECHI ZA LIGI KUU BARA, MBEYA CITY 2-SIMBA 0
AZAM FC 2- KAGERA SUGAR 1

KWA PICHA ZAIDI ZA MTANANGE HUU, KAA NASI BAADAYE.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.