Habari za Punde

*SIMBA YATEPETA TENA KWA MBEYA CITY, YAPIGWA 2-0 SOKOINE, AZAM FC YASHINDA

Kikosi cha Mbeya City. Picha na Maktaba ya Mafoto
***********************************************
Mbio za timu ya Simba Sc za kuwania nafasi ya pili katika ligi kuu ya Tanzania Bara ziliingia dosari baada ya kufungwa mabao 2-0 na timu ya Mbeya City.

Wakati Simba Sc ikipoteza kwenye uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya, wenzao wa Azam FC walichomoza na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Chamaz Complex na kufufua matumaini yake ya kuiwakilisha nchi katika moja ya mashindano ya CAF.

Azam Kwa sasa ina pointi 42, nne nyuma ya Yanga inayoongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 46. 

Hata hivyo Azam FC imeizidi Yanga mechi moja. 

Mbeya City ilicheza vizuri katika mchezo huo na mabao yake yalifungwa na Paul Nonga na Peter Malyanzi.  

Na kwa upande wa Azam Fc, mabao yake yalifungwa na Frank Domayo na Gaudence Mwaikimba, huku bao la mwaikimba likizua utata mkubwa.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.