Abiria wakiwa ndani ya usafiri wa Gari la mizigo maarufu kama Kirikuu, wakielekea katika mihangaiko yao ya kila siku kama walivyonaswa na kamera ya Mafoto maeneo ya Karume jijini Dar es Salaam, jana. Madereva wengi wenye magari ya mizigo aina hiyo na Pick up wamekuwa wakitoa huduma ya usafiri kwa abiria kuanzia juzi mabasi ya abiria yalipogoma, ambapo wamekuwa wakiwatoza kila abiria nauli ya sh. 500 Hadi 1000.
Safari ikiendelea mdogo mdogo.Kondakta akikusanya nauli yake kwa abiria wake.



No comments:
Post a Comment