Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiambatana na Katibu Mkuu
Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile
alipotembelea ofisi za Wizara ya Fedha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipata ufafanuzi kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile wakati wa ziara hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na uongozi wa Wizara ya Fedha.
**********************************
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TAARIFA KWA
VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe
Joseph
Magufuli amefany aziara ya kushtukiza katika Ofisi za Wizara ya Fedha leo Ijumaa tarehe 6
Novemba, 2015.
Katika ziara hiyo Mhe.Rais alipata fursa ya kutembelea baadhi ya Ofisi za Wizara na baadae kuzungumza na Viongozi wa Wizara ili kufahamu changamoto ambazo zinaikabili Wizara ya Fedha.
Wakati akimkaribisha Mhe.Rais Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt.
Servacius Likwelile alimueleza kuwa Wizara ya Fedha inakabiliwa na changamoto kubwa inayotokana na makusanyo ya mapato ya ndani.
Miongoni mwa sababu ni misamaha ya kodi, wafanyabiashara wengi hasa wakubwa kukwe pakodi,
makusanyo yasiyoridhisha ya maduhuli na kutokulipwa kwa kodi za majengo.Aidha Dkt.
Likwelile alishauri ni bora kuwekwa mifumo mizuri, ikiwemo matumizi ya Tehamana EFDs.
“Pamoja na ziara yangu kuwa ni ya kustukiza nimefurahi sana kukuta Viongozi wote wapo ofisini na wanafanyakazi. Jambo hili limenipa faraja kubwa. Ziara yangu
ya kuja hapa
nimejifunza na kujua changamoto zipi zinazowakabili”. Alisema Mhe. Rais.
Nimesikia changomoto nyingi naninaagiza kuwa muhakikishe walipakodi wakubwa wanalipa kodi na kusimamia kikamilifu Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA) ili iweze kukusanya kodi kikamilifu na sikuwabana wafanyabiashara wadogo wadogo.
Mhe.Rais aliwataka Viongozi wa Wizara kufanya kazi kwa bidii ili kuvuka lengo.
Imetolewana;
MsemajiwaWizarayaFedha
IngiahediC.Mduma
No comments:
Post a Comment