Habari za Punde

*MAZOEZI YA VITENDO WAKATI WA KUHITIMISHA MAFUNZO YA AWALI KWA WAHITIMU WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI YALIYOFANYIKA CHUO CHA UONGOZI JKT KIMBIJI

 Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, wakiwa wamebeba mfano wa majeruhi wa ajali, mara baada ya kumuokoa kutoka eneo la tukio wakati wa maonyesho ya kufunga mafunzo ya kozi ya awali ya  Sajini na Askari wa Jeshi hilo,yaliyofanyika Chuo cha Uongozi JKT Kimbiji,jijini Dar es Salaam, leo.
 Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, wakionyesha jinsi ya kuzima moto wakati wa maonyesho ya kufunga mafunzo ya kozi ya awali ya  Sajini na Askari wa Jeshi hilo,yaliyofanyika Chuo cha Uongozi JKT Kimbiji,jijini Dar.
 Wahitimu wakionyesha mafunzo ya karate waliyopata mara baada ya kuhitimu  kozi ya awali ya Sajini na Askari  wakati wa kufunga mafunzo hayo katika Chuo cha Uongozi JKT Kimbiji,jijini Dar
 Wahitimu wakionyesha mafunzo ya sarakasi  waliyopata mara baada ya kuhitimu  kozi ya awali ya Sajini na Askari  wakati wa kufunga mafunzo hayo katika Chuo cha Uongozi JKT Kimbiji,jijini Dar
 Mhitimu wa Mafunzo ya Kozi ya Awali ya Sajini na Askari,Joel Daniel(kulia),akimpiga teke mhitimu mwenzake Sylvestre Mandawa, wakati wa maonyesho ya karate ya  kufunga mafunzo ya kozi ya awali ya  Sajini na Askari wa Jeshi hilo,yaliyofanyika Chuo cha Uongozi JKT Kimbiji,jijini Dar
 Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,wakiwadhibiti vijana ambao ni mfano wa wezi ambao walikamatwa wakiiba vitu wakati wa janga la moto,maonyesho hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki,Chuo Cha Uongozi JKT Kimbiji
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil, akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya kozi ya awali ya Sajini na Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Chuo Cha Uongozi JKT Kimbiji
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Pius Nyambacha, akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya kozi ya awali ya Sajini na Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Chuo Cha Uongozi JKT Kimbiji,jijini Dar es Salaam.Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.