Habari za Punde

*NAIBU WAZIRI WA AFYA DKT.KIGWANGALA, AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA KLINIKI YA DKT. MWAKA

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwasili kituo cha tiba za asili na mbadala cha Kliniki ya Foreplan Herbal cha Dkt. Juma Mwaka leo jioni alipofanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho kilichopo eneo la Ilala Bungoni jijini Dar es salaam kujionea namna kituo hicho kinavyotoa huduma za kiafya.
  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangalla akiongea na Husna Maokola Majogo (aliyekaa) mara baada ya kuwasili kituo cha tiba za asili na mbadala cha Kliniki ya Foreplan Herbal cha Dkt. Juma Mwaka leo jioni alipofanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho kilichopo eneo la Ilala Bungoni jijini Dar es salaam kujionea namna kituo hicho kinavyotoa huduma za kiafya.
  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangalla akiangalia baadhi ya vifaa vinavyotumika kutibia wagonjwa katika kituo cha tiba za asili na mbadala cha Kliniki ya Foreplan Herbal cha Dkt. Juma Mwaka leo jioni alipofanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho kilichopo eneo la Ilala Bungoni jijini Dar es salaam kujionea namna kituo hicho kinavyotoa huduma za kiafya. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,wizara hiyo Nsachris Mwamwaja.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangalla akiangalia baadhi dawa zinavyotumika kutibia wagonjwa katika kituo cha tiba za asili na mbadala cha Kliniki ya Foreplan Herbal cha Dkt. Juma Mwaka leo jioni alipofanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho kilichopo eneo la Ilala Bungoni jijini Dar es salaam kujionea namna kituo hicho kinavyotoa huduma za kiafya.
  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangalla akiongea na baadi ya watoa huduma (waliovaa sare nyeusi) wakati wa ziara ya kushtukiza katika kituo cha tiba za asili na mbadala cha Kliniki ya Foreplan Herbal cha Dkt. Juma Mwaka kilichopo eneo la Ilala Bungoni jijini Dar es salaam. Wa kwanza kushoto ni Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,wizara hiyo Catherine Sungura.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangalla akipita kuangalia maeneo ya kutolea huduma katika kituo cha tiba za asili na mbadala cha Kliniki ya Foreplan Herbal cha Dkt. Juma Mwaka leo jioni alipofanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho kilichopo eneo la Ilala Bungoni jijini Dar es salaam kujionea namna kituo hicho kinavyotoa huduma za kiafya. Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO
*****************************************
Na Eleuteri Mangi -MAELEZO
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangalla ametoa siku saba kuchunguza kituo cha tiba za asili na mbadala cha Kliniki ya Foreplan Herbal kinachomilikiwa na Dkt. Juma Mwaka.
Dkt. Kigwangalla ametoa agizo hilo kufuatia ziara ya kushtukiza aliyoifanya katika kituo hicho kilichopo eneo la Ilala Bungoni jijini Dar es salaam kujionea namna kituo hicho kinavyotoa huduma za kiafya.
Dkt. Kigwangalla alifikia hatua hiyo ya uchunguzi baada ya mazingira ya mapokezi ya msafara wake kutopewa ushirikiano wakati wa ziara hiyo ambapo kulizua hali ya wasiwasi kwa watoa huduma wa kituoni hapo na ndipo alipomuagiza Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Tiba Asilia na tiba Mbadala Dkt. Mhame Paulo kufanya uchunguzi kupitia Baraza la Tiba Asilia kama kituo hicho kipo kisheria.
Katika hali isiyotarajiwa, viongozi na watoa huduma wa kituo hicho walipogundua kuna ugeni wa Naibu Waziri huyo waliacha ofisi zao na kutoweka kituoni hapo na hata waliokuwepo hawakuwa tayari kuzungumzia hali ya matibabu kituoni hapo.
“Mkurugenzi wa kituo hiki tunafahamu na alikuwepo hapa, amepanda gari dakika 10 kabla hatujaja hapa, Matabibu, wafamasia na watu wa vipimo wametoroshwa kupitia mlango wa nyuma tusionane nao kuona namna wanavyotoa huduma”,
“Sasa tambueni kuwa Serikali ipo na inafanya kazi yake, nitakuja tena wakati wowote ninaoujua mimi” alisisitiza Dkt. Kigwangalla.
Dkt. Kigwangalla amelitaka Baraza la Tiba Asilia kufanya uchunguzi ndani ya wiki moja kuibaini taaluma za watoa huduma kituoni hapo, aina ya miti shamba inayotumika kama dawa ili kujua kama Watanzania wanapata huduma halali na kama siyo halali Serikali ichukue hatua satahiki dhidi yao.
Aidha, Dkt. Kigwangalla ambaye pia ni Mtaaluma katika masuala ya afya kutoka Chuo Kikuu Cha Sayansi Na Tiba Muhimbili na Chuo Cha Karolinska cha nchini Sweden alisema Mkurugenzi wa kituo hicho amekosa weledi na anajiita “Dkt” Juma Mwaka, na kusisitiza kuwa miongoni mwa makosa ya kimaadili ya kidaktari wa kisasa na kujitangaza kupitia vyombo vya habari kitu ambacho ni kinyume na miiko ya taaluma hiyo.
Katika hatua nyingine, Dkt. Kigwangalla amemuagiza Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Tiba Asilia na Tiba Mbadala Dkt. Mhame Paulo kwa kushirikiana na Baraza la Tiba Asilia wafanye pia uchunguzi kwa Dkt. Rahabu Rubago anayetibu vidonda vya tumbo pamoja na Dkt Isack Ndodi anayetibu magonjwa mbalimbali kwa kutumia tiba mbadala na kupeleka taarifa hiyo ofisini kwa Naibu Waziri huyo ndani ya siku saba.
Kwa upande wake mmoja wa watoa huduma kituoni hapo Teddy Mbuya alisema kuwa yeye siyo msemaji, viongozi hawakuwepo ambapo alimuongoza Naibu Waziri maeneo mbalimbali kujionea hali ilivyo kwenye vyumba vya kutolea huduma za vipimo, mapokezi, duka la dawa asilia na sehemu ya kupumzika wagonjwa wakiwa wanasubiri kuhumiwa.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.