Habari za Punde

*RAIS DKT. MAGUFULI AELEZA MIKAKATI YA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA


Jacquiline Mrisho
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali ya Tanzania inatekeleza mikakati ya kuweka mazingira bora ili sekta isiyo rasmi iweze kuchangia vizuri katika maendeleo ya Taifa.
Mhe. Magufuli aliyasema hayo wakati akifungua Maonesho ya Wajasiriamali ya Juakali/Nguvu Kazi kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
Akifungua kwa niaba ya Rais, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Said Meck Sadiki alitaja mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuweka mpango maalumu wa kurasimisha shughuli za Sekta isiyo rasmi (MKURABITA).
Alisema mpango hu unatoa fursa ya mikopo nafuu kuwawezesha wajasiriamali na kuwapa elimuya namna bora ya kufungasha bidhaa zinazozalishwa.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Said Meck Sadiki maonesho hayo yameshirikisha wajasiriamali zaidi ya 700 kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Pia maonesho hayo wamehudhuriwa na Mabalozi kutoka nchi wanachama, Makatibu Wakuu,Wakurugenzi, Wenyeviti wa Wajasiriamali hao kutoka Nchi wanachama.
Maonesho hayo pia yameshirikisha Taasisi mbalimbali zikiwemo Taasisi za Fedha,Taasisi ya Mifuko ya Jamii na Mamlaka ya usajili (BRELA).
Kabla ya kufungua maonesho hayo, Mheshimiwa Said Meck  Sadiki  alitembelea baadhi ya mabanda ili kuona kazi za wajasiriamali hao.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Wajasiriamali Wasiorasimishwa Afrika Mashariki, Josephat Rweyemamu alisema madhumuni ya maonesho hayo ikiwemo kuwawezesha wajasiriamali kupanua masoko ya bidhaa zao pamoja na changamoto wanazozipata wajasiriamali hao.
Alieleza baadhi ya changamoto kuwa ni ukubwa wa kodi, pia aliiomba Serikali kufungua kiwanda cha Urafiki  ili kuwasaidia wajasiriamali pia kuwatengea maeneo maalum kwa ajili ya kufanyia biashara zao.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt Joyce Mapunjo alieleza kufurahishwa na bidhaa za wajasiriamali.
“Nimefurahishwa sana na  bidhaa  mbalimbali toka kwa wajasiriamali wa Afrika Mashariki na Serikali zetu za Afrika Mashariki zinatambua mchango wa Sekta isiyo rasmi na ndio mana tukawa na maonesho haya”.alisema Mhe. Dkt. Mapunjo.
Hata hivyo, alisema pamoja na mafanikio hayo, Serikali za nchi wanachama zinatambua kwamba Sekta isiyo rasmi inakabiliwa na vikwazo na changamoto nyingi ambazo zinadumaza maendeleo ya Sekta hii isiweze kukuwa na kuwa Sekta rasmi.
Rais John Pombe Magufuli amewahakikishia wajasiriamali wa Tanzania kuwa wameshayajadili na kwasasa wanayafanyia kazi.
“Kuna hatua ambayo Serikali ya Tanzania inatekeleza katika kuweka mazingira bora ili Sekta isiyo rasmi iweze kuchangia vizuri katika maendeleo ya Taifa letu” aliongeza.
 Maonesho hayo yalianzishwa tangu mwaka 1999 na hufanyika katika Nchi  za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mzunguko.
Kwa Tanzania haya ni maonesho ya Tano kufanyika na kauli mbiu ya mwaka huu ni “Nunua bidhaa zilizozalishwa na Afrika Mashariki ili kukuza uchumi wa Afrika Mashariki”.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.