Habari za Punde

*WAUZA VYAKULA KIHOLELA KUPELEKWA MAHAKAMANI

Na Skolastika Tweneshe  MAELEZO
Wafanyabiashara   wameaswa kutoendelea  na uuzaji wa  vyakula  na matunda yaliyomenywa  katika maeneo yaliyo wazi na yoyote atakayeendelea kuuza   atachukuliwa hatua  kali za kisheria hii ni kutokana na kuenea  kwa  ugonjwa wa kipindupindu.

Hayo  yamesemwa leo Jijini  Dar es salaam  na Msemaji wa Manispaa  ya  Ilala Bw. David  Langa  alipozungumza na mwandishi  kuhusu tamko  la Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee  na Watoto  Mhe.Ummy  Mwalimu  kupiga  marufuku uuzwaji  wa  vyakula  au matunda  yaliyomenywa  katika  maeneo ya wazi.

“Kwa mfanyabiashara yoyote  tutakayemkamata  tutamfikisha mahakamani  na  adhabu  yake  ni faini ya  sh 30,000 au kwenda jela miezi mitatu au vyote kwa  pamoja.”  alisema Langa.

Aidha Bw. David  Langa amesema katika  ukutekelezaji wa suala  hili watendaji wa kata  wanahusika moja kwa moja kusimamia na  kufuatilia kwa karibu operesheni hii, na kusisitiza sheria  za Afya kuzingatiwa  na kutokuwa na huruma kwa yeyote  atakayevunja sheria.

Kumekuwa  na uuzwaji wa  vyakula  na matunda yaliyomenywa jijini Dar es salaam hasa  maeneo ya katikati ya jiji hivyo kuhatarisha afya za wananchi, ila Serikali kupitia halmashauri zake imeahidi  kulitilia mkazo suala hili.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.