Habari za Punde

*MISS DAR INDIAN OCEAN 2016 WAKABIDHIWA GARI LA KUPIGIA MISELE

 Na Zainab Nyamka, Dar
MISS Dar Indian Ocean 2016 wamekabidhiwa gari na kampuni ya Helmic Group Company Limited ikiwa ni maandalizi kuelekea shindano hilo linalotarajiwa kufanyika hivi karibuni. 
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi gari hilo aina ya Coaster litakalokuwa linatumika kwa ajili ya kuwapeleka warembo hao sehemu mbalimbali, Msemaji na mratibu wa warembo hao Sarah Martin ameshukuru kwa hatua hiyo kutoka Helmic  na kusema kuwa hiyo ni hatua nzuri kwao kwani kwa warembo waliopo wana uhakika wa kulibakiza taji la Miss Tanzania kutoka Miss Dar Indian Ocean. 
"Kutoka Miss Dar Indian Ocean tumeweza kutoa warembo mbalimbali na waliweza kuwa Miss Tanzania na hilo tunajivunia sana kwani ukiangalia Nancy Sumari, Wema Sepetu, Richa Adhia na Faraja Kota wote walitokea hapa,".
Aidha alisema kuwa, moja ya malengo yao makubwa  ni kuweza kuwasaidia warembo wao kufika mbali hususani kwenye masuala ya urembo.
''Ukizingatia tuna kampuni inayojihusisha na mitindo basi hatutaweza kuona wanaishia hapa na kupotea zaidi tutawachukua na kufanya nao kazi zaidi ya hapa. 
Mkurugenzi Mtendaji wa kampini ya Helmic Group Harprit Kaur Sohal alisema kuwa huu ni mwanzo ila malengo yao makubwa ni kuwasaidia warembo hao katika shindano lao Miss la Dar Indian Ocean na zaidi wamewapatia gari hilo kwa ajili ya kuwarahisishia kwenye shindano lao na amewataka warembo kujiamini zaidi. 
Mshiriki wa Dar Indian Ocean, Neema Steven Dismas amesema kuwa akifanikiwa kushinda taji hilo ana imani atazidi kuiwakilisha nchi yetu vizuri hasa akiweza kwenda kwenye mashindano ya kimataifa kwa kutumia nembo ya Taifa ambayo ni Mlima Kilimanjaro, Mbuga za wanyama na lugha adhimu ya kiswahili.

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.