Mabekiwa Yanga Hassan Kessy (kushoto) na Nadir Haroub, wakishangilia kwa furaha baada ya mwamuzi kupuliza filimbi ya mwisho katika mchezo wao dhidi ya Mbeya City, jana ambapo Yanga waliibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 2-1 na kurudi kileleni mwa ligi wakiwashusha mahasimu wao Simba kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa huku pointi wakiwa sawa.
**********************************************
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara Dar Young Africans, jana wamekaa tena kileleni mwa Ligi hiyo baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo mabingwa hao watetezi sasa wamefikisha pointi 65 wakicheza mechi 28 wakibakiza mechi mbili mkononi na kuongoza Ligi hiyo.
Mahasimu wao Simba wamerudi nafasi ya pili huku wao pia wakiwa na pointi zake 65 na mechi 29, wakibakiza mechi moja mkononi.
Bao la Yanga lilifungwa na winga Simon Msuva kwa kichwa dakika ya saba tu akimalizia krosi ya Hassan Kessy.

Mshambuliaji wa Yanga Obrey Chirwa (kulia) akichuana kuwania mpira nabeki wa Mbey City, Tumba Lui.
***********************************************
Baada tu ya Msuva kufunga bao hilo, hakuweza kushangilia bao lake wala kuendelea na mchezo, kutokana na kuumia na kupasuka paji la uso juu ya jicho la kulia alipogongana na beki wa Mbeya City, Tumba Lui na nafasi yake ikichukuliwa na beki Juma Abdul.
Kwa mabadiliko hayo, Kessy alikwenda kucheza kama winga wa kulia juu ya Abdul Abdul huku wakipokezana kuzuia na kushambulia.
Kessy akimkalisha Mwasapile
*********************************************
Yanga walipata bao la pili lililofungwa na mshambuliaji, Obrey Chirwa dakika ya 64 akimalizia mpira wa adhabu wa Juma Abdul.
Mrisho Ngassa aliingia kipindi cha pili upande wa Mbeya City, lakini hakuwa na madhara kwa timu ya yake ya zamani zaidi tu ya kusisimua mashabiki kwa uchezaji wake wa kuranda pande zote za uwanja.
KIKOSI CHA YANGA: Benno Kakolanya, Hassan Kessy/Emmanuel Martin dk, Mwinyi Hajji Mngwali, Vincent Bossou, Nadir Haroub ‘Cannavaro’/Kevin Yondan dk67, Thabani Kamusoko, Simon Msuva/Juma Abdul dk12, Haruna Niyonzima, Amisi Tambwe, Obrey Chirwa na Geoffrey Mwashiuya.
Chirwa (Kulia) akichuana na Tumba
Chirwa akishangilia bao lake huku akipongezwa na Emmanuel Martin
Chirwa akimtoka beki wa Mbeya City, Hassan Mwasapile.
Hassan Kessy akimtoka Mwasapile....
Hassan Kessy akimtoka Majaliwa Shaban
Hassan Kessy akiwatoka mabeki wa Mbeya City
Kessy akipiga krosi
Kipa wa Mbeya City, Owen Chaima, akiruka kujaribu kupangua mpira uliopigwa kwa kichwa na Amis Tambwe na mshinda baada ya kugonga mwamba.


Shabiki wa Yanga akishangilia kwa staili ya kuonyesha Kipolo
Mashabiki wa Yanga wakilaumu baadhi ya matukio ya uwanjani
Simon Msuva akimramba chenga beki wa Mbeya City, Sankani Mkandawile
Msuva akiwania mpira na Lui
Msuva akiwatoka mabeki wa Mbeya City
Msuva akiwatoka mabeki wa Mbeya City
Geofrey Mwashiuya (kulia) akichuana na Rajab Isihaka
Haji Mwinyi (kulia) akichuana na Rajab Isihaka
Mrisho Ngassa akimiliki mpira
Niyonzima akimtoka beki wa Mbeya City
Niyonzima akipiga krosi
Amis Tambwe akimiliki mpira katikati ya mabeki wa Mbeya City
No comments:
Post a Comment